DRC

Uhusiano wa kidiplomasia matatani kati ya DRC na Kongo Brazaville

JULAI 30, 2023
Border
news image

Waziri Mkuu wa Kongo ya Kidemkrasia na mwenziye wa Kongo Brazaville wakutana kumaliza tofauti bahina ya mataifa yao.

Mkutano wao uliofanyika Pembezoni wa michezo ya Olimpiki , inayo shirikisha mataifa zinazo tumia kifaransa kama lugha rasmi Duniani jijini Kinshasa Mji mkuu wa Kongo ya Kidemkrasia . Waziri Mkuu wa DRC Bw. Sama Lukonde na mwenziye wa Kongo Brazaville Bw. Makosso Anatole walikutana kwa mazungumzo , katika kile kinacho elezwa kama kuchunguza mwenendo wa hali ya kidiplomasia kati ya mataifa hayo jirani katika kanda ya Afrika ya kati.

Kupitia akaunti yake ya twitter , waziri wa habari na msemaji wa serikali ya DRC Bw. Patric Muyaya , ame fafanua kwamba mawaziri hao wali papasia pia namna gani , kusukuma mbele miradi zao za pamoja kati ya Kinshasa na Brazaville.

Austere Malivika - MTV