DRC
DRC Wakimbizi wa Vita mashariki mwa Congo waomba kurejea
nyumbani kutokana na mateso wanao pitia katika kambi mbali
mbali .
Wakishudia mvua kali kwa sasa katika hema zao ambako waishi
katika kambi mbali ,wakimbizi wa vita mashariki mwa Congo
waomba kurejeshwa kwenye vijiji vyao kwani wamechoka na
Maisha ya kuishi katika hema . Mmmoja wa wkaimbizi alie
hifadhi jina lake asema ,kwa sasa amejikuta na maradhi ya
msongo wa mawazo kutokana na Maisha anayo ishi kwa sasa
akiwa na Watoto kambini bila kusoma . Mama huyu anasema kila
siku anaondoka asubui kambini kutafuta kuni katika mbuga la
Wanyama pori la Virunga pembeni ya kambi yake ya Bulengo
lakini hukutana na watu wenye silaha wanao baka wanawake.