DRC - BENI

Watu 25 wameokolewa baada ya mapigano na mashambulizi makali iliyoendeshwa na jeshi la serikali ya Congo FARDC dhidi ya wapiganaji kutoka kundi la ADF katika kijijini Tingwe wilayani Beni

AGOSTI 22, 2023
Border
news image

Ni watu 25 kati yao watoto 9 ndio wameokolewa na Jeshi la Kongo FARDC usiku wa kuamkia juma nne Ogasti 22 kijijini Tingwe kinacho patikana kunako kilomita 70 kaskazini mashariki mwa Mji Beni Kivu kaskazini .

Raia walio okolewa , walitekwa na waasi katika mashambulizi mbalimbali kati ya mwaka 2016 na 2023 , Kepten Antony mwalushay msemaji wa operesheni sukula1 katika maeneo ya Beni Lubero

"Tuna dhibiti hali ya mambo tangu jana majira ya mchana , sababu askari wetu waliokuwa waki fuatilia adui wali pambana naye , tuli fanikiwa kukomboa raia walio tekwa . Askari wetu wana endelea na Doria ya vita katika eneo hilo kuelekea musituni ambako adui ali kimbilia "

kati yao kuna pia wanaume ila idadi kubwa ni wanawake ; asema Rachid MALIRO kiongozi wa Kiraia katika Mji Mdogo wa Eringeti .

"Afya yao ina dhoofika sana kwa watoto na wanawake , kuna watoto wa umri wa miaka 2 , 3 , 4 , wame eleza ya kwamba shamba ambayo ADF ilifanya katika mtandao wa barabara ya Eringeti Kainama , watoto 4 wa jamaa moja wali shuhudia kwamba Mama yao ali chinjwa kama mbuzi kwa pori , Fardc imeweza kutosha hizi jamaa zote kwa mikono ya hao wauni "

Ogasti 20, Jeshi la Fardc lilipambana tena na waasi hao kwenye mpaka wa mkoa wa kivu kaskazini na Ituri kijijini Baungatsu Luna karibu na mji wa Eringeti , watu 6 walifariki miongoni watuhumiwa adf 3 kwa mujibu wa duru za kijeshi .

MTV NEWS