Julien Paluku waziri wa viwanda na mwana siasa maarfu nchini aomba uongozi wa kijeshi kuondoshwa Ituri na Kivu Kaskazini na kuweka kambi mpya ya kijeshi eneo la Beni ambako wanajeshi lazima wapambane na waasi wa ADF kwani swala la uongozi ni la wananchi yaani raia.
Kwa Mtazamo wake kama mtafiti, anatumia muda wake mrefu katika utawala wa eneo hilo ili kuweka kwenye meza ya tume hizo tatu vipengele vinavyoweza kutumiwa huko kwa ajili ya kujitajirisha. Kahongya amesema kwamba wananchi wameomba Rais kuchukuwa hatua mpya na kuwapa kazi nyingine wanajeshi kwani swala la utawala wameshindwa ,na kabla ya mutu kupewa nyazifa za utawala lazima kufunzwa kwanza.
Mashirika ya kiraia ,wabunge mbali mbali toka Ituri na Kivu kaskazini wote wakiomba kuondoa magavana wa kijeshi na kurejesha utawala wa magavana walio chaguliwa na wananchi.